1
1 Wafalme 17:14
Neno: Bibilia Takatifu
Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo BWANA, Mungu wa Israeli: ‘Lile gudulia la unga halitakwisha wala ile chupa ya mafuta haitakauka hadi siku ile BWANA atakapoleta mvua juu ya nchi.’ ”
Compare
Explore 1 Wafalme 17:14
2
1 Wafalme 17:1
Basi Eliya, Mtishbi kutoka Tishbi katika Gileadi, akamwambia Ahabu, “Kama BWANA, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninamtumikia, hapatakuwa na umande wala mvua katika miaka hii, isipokuwa kwa neno langu.”
Explore 1 Wafalme 17:1
3
1 Wafalme 17:13
Eliya akamwambia, “Usiogope. Nenda nyumbani ukafanye kama ulivyosema. Lakini kwanza unitengenezee mimi mkate mdogo kutoka vile ulivyo navyo kisha uniletee na ndipo utayarishe chochote kwa ajili yako na mwanao.
Explore 1 Wafalme 17:13
4
1 Wafalme 17:12
Akamjibu, “Hakika kama BWANA Mungu wako aishivyo, sina mkate wowote, isipokuwa konzi ya unga kwenye gudulia na mafuta kidogo kwenye chupa. Ninakusanya kuni chache nipeleke nyumbani na nikapike chakula kwa ajili yangu na mwanangu, ili kwamba tule, kiishe, tukafe.”
Explore 1 Wafalme 17:12
5
1 Wafalme 17:9
“Ondoka, uende Sarepta ya Sidoni na ukae huko. Nimemwagiza mjane katika sehemu ile akupatie chakula.”
Explore 1 Wafalme 17:9
6
1 Wafalme 17:16
Kwa kuwa lile gudulia la unga halikwisha na ile chupa ya mafuta haikukauka, sawasawa na lile neno la BWANA alilosema Eliya.
Explore 1 Wafalme 17:16
7
1 Wafalme 17:15
Akaondoka na kufanya kama Eliya alivyomwambia. Kwa hiyo kukawa na chakula kila siku kwa ajili ya Eliya, yule mwanamke na jamaa yake.
Explore 1 Wafalme 17:15
8
1 Wafalme 17:10
Hivyo akaenda Sarepta. Alipofika kwenye lango la mji, mjane alikuwa huko akiokota kuni. Akamwita na kumwambia, “Naomba uniletee maji kidogo kwenye gudulia ili niweze kunywa.”
Explore 1 Wafalme 17:10
9
1 Wafalme 17:4
Utakunywa maji kutoka kile kijito, nami nimeagiza kunguru wakulishe huko.”
Explore 1 Wafalme 17:4
10
1 Wafalme 17:11
Alipokuwa anakwenda kumletea, akamwita akasema, “Tafadhali niletee pia kipande cha mkate.”
Explore 1 Wafalme 17:11
11
1 Wafalme 17:6
Kunguru wakamletea mkate na nyama asubuhi na mkate na nyama jioni, naye akanywa maji kutoka kile kijito.
Explore 1 Wafalme 17:6
12
1 Wafalme 17:7
Baada ya muda, kile kijito kikakauka kwa sababu mvua haikuwa imenyesha katika nchi.
Explore 1 Wafalme 17:7
13
1 Wafalme 17:24
Ndipo yule mwanamke akamwambia Eliya, “Sasa ninajua kwamba wewe ni mtu wa Mungu, na kwamba neno la BWANA kutoka kinywani mwako ni kweli.”
Explore 1 Wafalme 17:24
14
1 Wafalme 17:5
Hivyo akafanya kile alichoambiwa na BWANA. Akaenda katika Kijito cha Kerithi, mashariki ya Yordani na akakaa huko.
Explore 1 Wafalme 17:5
15
1 Wafalme 17:22
BWANA akasikia kilio cha Eliya, na roho ya kijana ikamrudia, naye akafufuka.
Explore 1 Wafalme 17:22
Home
Bible
Plans
Videos