1
Mhubiri 5:2
Neno: Bibilia Takatifu
Usiwe mwepesi kuzungumza, usiwe na haraka katika moyo wako kuzungumza lolote mbele za Mungu. Mungu yuko mbinguni nawe uko duniani, kwa hiyo maneno yako na yawe machache.
Compare
Explore Mhubiri 5:2
2
Mhubiri 5:19
Zaidi ya yote, Mungu anapompa mtu yeyote utajiri na milki, humwezesha kuvifurahia, kukubali fungu lake na kuwa na furaha katika kazi yake, hii ni karama ya Mungu.
Explore Mhubiri 5:19
3
Mhubiri 5:10
Yeyote apendaye fedha kamwe hatosheki na fedha; yeyote apendaye utajiri kamwe hatosheki na kipato chake. Hili nalo pia ni ubatili.
Explore Mhubiri 5:10
4
Mhubiri 5:1
Linda hatua zako uendapo katika nyumba ya Mungu. Karibia usikilize kuliko kutoa dhabihu ya wapumbavu, ambao hawajui kuwa wanafanya kosa.
Explore Mhubiri 5:1
5
Mhubiri 5:4
Wakati unapomwekea Mungu nadhiri, usikawie kuitimiza. Yeye hafurahii wapumbavu; timiza nadhiri yako.
Explore Mhubiri 5:4
6
Mhubiri 5:5
Ni afadhali usiweke nadhiri kuliko kuiweka na usiitimize.
Explore Mhubiri 5:5
7
Mhubiri 5:12
Usingizi wa kibarua ni mtamu, awe amekula kidogo au kingi, lakini wingi wa mali humnyima tajiri usingizi.
Explore Mhubiri 5:12
8
Mhubiri 5:15
Mtu hutoka tumboni mwa mama yake uchi, naye jinsi alivyokuja vivyo hivyo huondoka. Hachukui chochote kutokana na kazi yake ambacho anaweza kukibeba mkononi mwake.
Explore Mhubiri 5:15
Home
Bible
Plans
Videos