1
Isaya 25:1
Neno: Bibilia Takatifu
Ee BWANA, wewe ni Mungu wangu, nitakutukuza na kulisifu jina lako, kwa maana katika ukamilifu wa uaminifu umetenda mambo ya ajabu, mambo yaliyokusudiwa tangu zamani.
Compare
Explore Isaya 25:1
2
Isaya 25:8
yeye atameza mauti milele. BWANA Mwenyezi atafuta machozi katika nyuso zote; ataondoa aibu ya watu wake duniani kote. BWANA amesema hili.
Explore Isaya 25:8
3
Isaya 25:9
Katika siku ile watasema, “Hakika huyu ndiye Mungu wetu; tulimtumaini, naye akatuokoa. Huyu ndiye BWANA, tuliyemtumaini; sisi tushangilie na kufurahia katika wokovu wake.”
Explore Isaya 25:9
4
Isaya 25:7
Juu ya mlima huu ataharibu sitara ihifadhiyo mataifa yote, kile kifuniko kifunikacho mataifa yote
Explore Isaya 25:7
5
Isaya 25:6
Juu ya mlima huu BWANA Mwenye Nguvu Zote ataandaa karamu ya vinono kwa mataifa yote, karamu ya mvinyo wa zamani, nyama nzuri sana na divai zilizo bora sana.
Explore Isaya 25:6
Home
Bible
Plans
Videos