1
Flp 4:6
Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia
Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
Compare
Explore Flp 4:6
2
Flp 4:7
Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.
Explore Flp 4:7
3
Flp 4:8
Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.
Explore Flp 4:8
4
Flp 4:13
Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
Explore Flp 4:13
5
Flp 4:4
Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.
Explore Flp 4:4
6
Flp 4:19
Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu.
Explore Flp 4:19
7
Flp 4:9
Mambo mliyojifunza kwangu na kuyapokea, na kuyasikia na kuyaona kwangu, yatendeni hayo; na Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.
Explore Flp 4:9
8
Flp 4:5
Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu.
Explore Flp 4:5
9
Flp 4:12
Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na katika mambo yo yote, nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na kupungukiwa.
Explore Flp 4:12
10
Flp 4:11
Si kwamba nasema haya kwa kuwa nina mahitaji; maana nimejifunza kuwa radhi na hali yo yote niliyo nayo.
Explore Flp 4:11
Home
Bible
Plans
Videos