1
Isaya 1:18
Biblia Habari Njema
Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Njoni, basi, tuhojiane. Ingawa mna madoa mekundu ya dhambi, mtatakaswa na kuwa weupe kama theluji; madoa yenu yajapokuwa mekundu kama damu, mtakuwa weupe kama sufu.
Compare
Explore Isaya 1:18
2
Isaya 1:19
Mkiwa tayari kunitii, mtakula mazao mema ya nchi.
Explore Isaya 1:19
3
Isaya 1:17
jifunzeni kutenda mema. Tendeni haki, ondoeni udhalimu, walindeni yatima, teteeni haki za wajane.”
Explore Isaya 1:17
4
Isaya 1:20
Lakini mkikaidi na kuniasi, mtaangamizwa kwa upanga. Mimi, Mwenyezi-Mungu, nimesema.”
Explore Isaya 1:20
5
Isaya 1:16
Jiosheni, jitakaseni; ondoeni uovu wa matendo yenu mbele yangu. Acheni kutenda maovu
Explore Isaya 1:16
6
Isaya 1:15
“Mnapoinua mikono yenu kuomba nitauficha uso wangu nisiwaone. Hata mkiomba kwa wingi sitawasikia, maana mikono yenu imejaa damu.
Explore Isaya 1:15
7
Isaya 1:13
Msiniletee tena matoleo yenu yasiyo na maana; ubani ni chukizo kwangu. Acheni kufanya sikukuu za mwezi mpya, Sabato na mikutano mikubwa ya ibada; sikubali ibada zilizochanganyika na dhambi.
Explore Isaya 1:13
8
Isaya 1:3
Ngombe humfahamu mwenyewe, punda hujua kibanda cha bwana wake; lakini Waisraeli hawajui, watu wangu, hawaelewi!”
Explore Isaya 1:3
9
Isaya 1:14
Sikukuu zenu za mwezi mpya na nyinginezo moyo wangu wazichukia. Zimekuwa mzigo mzito kwangu, nami nimechoka kuzivumilia.
Explore Isaya 1:14
Home
Bible
Plans
Videos