1
Ufunuo 2:4
Biblia Habari Njema
Lakini ninalo jambo moja dhidi yako: Wewe hunipendi tena sasa kama pale awali.
Compare
Explore Ufunuo 2:4
2
Ufunuo 2:5
Basi, pakumbuke pale ulipokuwa kabla ya kuanguka, ukatubu na kufanya kama ulivyofanya pale awali. La sivyo, naja kwako na kukiondoa kinara chako cha taa mahali pake.
Explore Ufunuo 2:5
3
Ufunuo 2:10
Usiogope hata kidogo yale ambayo itakulazimu kuteseka. Sikiliza! Ibilisi anataka kuwajaribu kwa kuwatia baadhi yenu gerezani; nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Muwe waaminifu hata mpaka kufa, nami nitawapeni taji ya uhai.
Explore Ufunuo 2:10
4
Ufunuo 2:7
“Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Mshindi nitamjalia kula matunda ya mti wa uhai ulioko ndani ya bustani ya Mungu.
Explore Ufunuo 2:7
5
Ufunuo 2:2
Najua mambo yako yote; najua bidii yako na uvumilivu wako. Najua kwamba huwezi kuwavumilia watu waovu, na kwamba umewapima wale wanaojisemea kuwa mitume na kumbe sio, ukagundua kwamba ni waongo.
Explore Ufunuo 2:2
6
Ufunuo 2:3
Wewe unayo saburi, umestahimili taabu nyingi kwa ajili ya jina langu, wala hukuvunjika moyo.
Explore Ufunuo 2:3
7
Ufunuo 2:17
“Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Mshindi nitampa ile mana iliyofichika. Nitampa pia jiwe jeupe lililoandikwa jina jipya ambalo hakuna mtu aliyelijua isipokuwa tu wale wanaolipokea.
Explore Ufunuo 2:17
Home
Bible
Plans
Videos