YouVersion Logo
Search Icon

Filemoni Utangulizi

Utangulizi
Waraka huu mfupi umeainishwa na nyaraka za Waefeso, Wakolosai na Wafilipi kama mojawapo wa nyaraka Paulo alizoandika akiwa gerezani. Aliandikia Filemoni, Afia mwanamke Mkristo (ambaye huenda alikuwa mkewe Filemoni), na Arkipo, na kanisa lililokuwa likikusanyika nyumbani kwa Filemoni.
Onesimo alikuwa mtumwa aliyetoroka kutoka kwa Filemoni huko Kolosai akaenda Rumi, ambako aliokoka. Onesimo, kama mtumwa, alikuwa mali ya Filemoni kisheria.
Mwandishi
Mtume Paulo.
Kusudi
Kumhimiza Filemoni amsamehe Onesimo, mtumwa aliyemtoroka, na amkubali kama ndugu Mkristo katika imani.
Mahali
Rumi.
Tarehe
Kama mwaka wa 60 B.K.
Wahusika Wakuu
Paulo, Filemoni, na Onesimo.
Wazo Kuu
Paulo alimwandikia Filemoni kumshawishi amkubali Onesimo kurudi kwake, na amsamehe aliyomkosea.
Mambo Muhimu
Barua hii ni kielelezo cha ukarimu wa Kikristo. Paulo alishukuru kwa moyo wa ukarimu ambao tayari Filemoni alikuwa ameonyesha kwa Wakristo wenzake. Paulo kwa mamlaka yake ya kitume katika kanisa angeweza kumtaka afanye hivyo kwa Onesimo. Badala yake Paulo aliomba kwa upendo Filemoni ampokee Onesimo.
Mgawanyo
Salamu (1-3)
Kuhusika kwa Paulo, na upendo wake (4-7)
Paulo kumwombea Onesimo (8-22)
Kuagana (23-25).

Currently Selected:

Filemoni Utangulizi: NEN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in