YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 4

4
Zaburi 4
Sala Ya Jioni Ya Kuomba Msaada
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Daudi.
1 Nijibu nikuitapo,
Ee Mungu wangu mwenye haki!
Nipumzishe katika shida zangu;
nirehemu, usikie ombi langu.
2 Enyi watu, mtabadilisha utukufu wangu
kuwa aibu mpaka lini?
Mtapenda udanganyifu
na kufuata miungu ya uongo mpaka lini?
3 Fahamuni hakika kwamba Bwana amewatenga
wale wamchao kwa ajili yake;
Bwana atanisikia nimwitapo.
4 Katika hasira yako, usitende dhambi.
Mkiwa vitandani mwenu, mtulie kimya
mkiichunguza mioyo yenu.
5 Toeni dhabihu zilizo haki;
mtegemeeni Bwana.
6 Wengi wanauliza, “Ni nani awezaye
kutuonyesha jema lolote?”
Ee Bwana, tuangazie nuru ya uso wako.
7 Wewe umejaza moyo wangu kwa furaha kubwa
kuliko watu waliopata nafaka na divai kwa wingi.
8 Nitajilaza chini na kulala kwa amani,
kwa kuwa wewe peke yako, Ee Bwana,
waniwezesha kukaa kwa salama.

Currently Selected:

Zaburi 4: NEN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in