YouVersion Logo
Search Icon

Ezekieli 2

2
Maono ya gombo
1 # Dan 10:11 Akaniambia, Mwanadamu, simama kwa miguu yako, nami nitasema nawe. 2#Hes 11:25; Amu 13:25; Neh 9:30; Eze 3:24; Yoe 2:28,29 Naye aliposema nami, roho ikaniingia, ikanisimamisha; nikamsikia yeye aliyesema nami. 3#Yer 3:25 Akaniambia, Mwanadamu, nakutuma kwa wana wa Israeli, kwa mataifa wanaoasi, walioniasi mimi; wao na baba zao wameasi juu yangu, naam, hata hivi leo. 4#Eze 3:7 Na wana hao wana nyuso zisizo na haya, na mioyo yao ni migumu. Mimi nakutuma kwa hao; nawe utawaambia, Bwana MUNGU asema hivi. 5#Eze 3:11; 33:33 Nao, iwe watasikia au hawataki kusikia, (maana ndio nyumba ya kuasi hao), hata hivyo watajua ya kuwa nabii amekuwako miongoni mwao. 6#Mt 10:28; Ebr 11:27; 1 Pet 3:14; Eze 3:26,27 Na wewe, mwanadamu, usiwaogope hao, wala usiyaogope maneno yao, ijapokuwa miiba na michongoma inakuzunguka, nawe unakaa katikati ya nge; usiyaogope maneno yao, wala usifadhaike kwa sababu ya nyuso zao, wajapokuwa ni nyumba yenye kuasi. 7#Yer 1:7,17; Mt 28:20 Nawe utawaambia maneno yangu, iwe watasikia au hawataki kusikia; maana hao wanaasi sana. 8#Ufu 10:9 Bali wewe, mwanadamu, sikia neno hili ninalokuambia; usiwe wewe mwenye kuasi kama nyumba ile yenye kuasi; funua kinywa chako, ule nikupacho. 9#Yer 1:9; Eze 3:1; Ufu 5:1 Nami nilipotazama, mkono ulinyoshwa kunielekea; na tazama, gombo la kitabu lilikuwa ndani yake. 10#Isa 3:11 Akalikunjua mbele yangu; nalo lilikuwa limeandikwa ndani na nje; ndani yake yalikuwa yameandikwa maombolezo, na vilio, na ole!

Currently Selected:

Ezekieli 2: SRUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in