YouVersion Logo
Search Icon

Kutoka 15:23-25

Kutoka 15:23-25 BHN

Walipofika mahali panapoitwa Mara, hawakuweza kuyanywa maji ya Mara kwa sababu yalikuwa machungu. Kwa sababu hiyo mahali hapo pakaitwa Mara. Basi, watu wote wakamlalamikia Mose wakisema, “Sasa tutakunywa nini?” Hapo Mose akamlilia Mwenyezi-Mungu, naye akamwonesha kipande cha mti, na Mose akakitumbukiza katika maji; maji hayo yakawa mazuri. Huko Mungu aliwapa Waisraeli amri na agizo, ili ajue uthabiti wao