YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 112

112
Furaha ya mtu mwema
1Msifuni Mwenyezi-Mungu!
Heri mtu anayemcha Mwenyezi-Mungu,
anayefurahia sana kutii amri zake.
2Wazawa wake watakuwa wenye nguvu nchini;
watoto wa wanyofu watapata baraka.
3Nyumbani kwake kutakuwa na mali nyingi;
uadilifu wake wadumu milele.
4Mtu mwema huangaziwa mwanga gizani;
mtu mwenye huruma, mpole na mwadilifu.
5Mtu mkarimu akopeshaye bila faida, hufanikiwa;
mtu afanyaye shughuli zake kwa kutumia haki.
6Mwadilifu hatashindwa kamwe,
huyo atakumbukwa milele.
7Hana haja ya kuogopa akipata habari mbaya;
ana moyo thabiti na humtegemea Mwenyezi-Mungu.
8Yuko imara moyoni, wala hataogopa;
naye atawaona maadui zake wanashindwa.
9 # Taz 2Kor 9:9 Hutoa kwa ukarimu, huwapa maskini;
uadilifu wake wadumu milele.
Nguvu yake inatukuzwa kwa heshima.
10Watu waovu huona hayo na kuudhika;
husaga meno kwa chuki na kutoweka,
matazamio ya mtu mbaya huishia patupu.

Currently Selected:

Zaburi 112: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in