YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 114

114
Mungu na watu wake
1Watu wa Israeli walipotoka Misri,
wazawa wa Yakobo walipotoka ugenini,
2Yuda ikawa maskani ya Mungu,
Israeli ikawa milki yake.
3Bahari iliona hayo ikakimbia;
mto Yordani ukaacha kutiririka!
4Milima ilirukaruka kama kondoo dume;
vilima vikaruka kama wanakondoo!
5Ee bahari, imekuwaje hata ukakimbia?
Nawe Yordani, kwa nini ukaacha kutiririka?
6Enyi milima, mbona mliruka kama kondoo dume?
Nanyi vilima, mmerukaje kama wanakondoo?
7Tetemeka, ee dunia mbele yake Mwenyezi-Mungu;
tetemeka mbele ya Mungu wa Yakobo,
8anayeugusa mwamba ukawa bwawa la maji,
nayo majabali yakawa chemchemi za maji!

Currently Selected:

Zaburi 114: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in