YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 23

23
Mungu mchungaji wangu
(Zaburi ya Daudi)
1Mwenyezi-Mungu ni mchungaji wangu,
sitapungukiwa na kitu.
2Hunipumzisha kwenye malisho mabichi;
huniongoza kando ya maji matulivu,
3na kuirudishia nafsi yangu nguvu mpya.
Huniongoza katika njia sawa
kwa hisani yake.
4Nijapopita katika bonde la giza kuu la kifo,
sitaogopa hatari yoyote,
maana wewe ee Mwenyezi-Mungu u pamoja nami;
gongo lako na fimbo yako vyanilinda.
5Umeniandalia karamu mbele ya maadui zangu;
umenipaka mafuta kichwani pangu;
kikombe changu umekijaza mpaka kufurika.
6Kweli wema wako na fadhili zako zitakuwa pamoja nami,
siku zote za maisha yangu;
nami nitakaa nyumbani mwa Mwenyezi-Mungu milele.

Currently Selected:

Zaburi 23: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in