Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Rum 8:39

Wimbo Wa Neema
Siku 5
Gundua undani wa upendo wa Mungu kwako kupitia ibada hii ya Wimbo wa Neema. Mwinjilisti Nick Hall atakuongoza kupitia ibada yenye nguvu ya siku 5 akikualika kujiunga na Wimbo wa neema ya Mungu unaoimbwa juu yako.

Mbona Mungu ananipenda?
Siku 5
Maswali: Ikija kwa Mungu, tuna maswali mengi sana. Kwa sababu ya tamaduni zetu, swali moja ambalo tutajipata tukijiuliza ni, "Mbona Mungu ananipenda?" au "Ni vipi atanipenda?" Mpango huu unashirikisha jumla ya vifungu 26 vya Biblia—Kila kifungu kikiongea juu ya upendo wa Mungu usiokuwa na shaka.

Yesu: Bendera Wetu wa Ushindi
Siku 7
Tunapo sherehekea Pasaka, tunasherehekea ushindi mkuu katika historia. Kupitia kifo cha Yesu na kufufuka, alishinda nguvu ya dhambi na kaburi, na athari zake zote, na alichagua kushiriki ushindi huo nasi. Pasaka hii, hebu tuangalie baadhi ya ngome alizozishinda, angalia vita alivyovipiga kwa ajili yetu, na umsifu kama bendera ya ushindi wetu.

Ibada juu ya Vita vya Akilini
Siku 14
Hii ibada itakusaidia kwa himizo za tumaini la kushinda hasira, machafuko, hukumu, hofu, shaka ... chochote kile. Ufahamu huu utakusaidia kujua njama ya adui ya kukuchanganya na kukudanganya, kukabiliana na mwelekeo wa mawazo ulioharibika, kupata ushindi katika kubadilisha mawazo yako, kupata nguvu, kutiwa moyo na, muhimu zaidi, ushindi juu ya kila vita akilini mwako. Una nguvu ya kupigana ... hata ikiwa ni siku moja kwa wakati!

BibleProject | Ufalme Unaoenda Kinyume na Matarijio / Sehemu ya 1 - Luka
Siku 20
Shirika la BibleProject liliandaa mwongozo wa Ufalme Unaoenda Kinyume na Matarijio Sehemu ya 1 kuwahimiza watu binafsi, vikundi vidogo na familia kusoma kitabu chote cha Luka kwa siku 20. Mwongozo huu unajumuisha video za katuni, muhtasari wa uchambuzi na maswali ya kutafakari ili kuwasaidia wahusika kumfahamu Yesu na kufuatilia mtiririko wa mawazo ya Luka pamoja na kuyaelewa mafunzo yake.

BibleProject | Tafakari ya Ujio wa Yesu
Siku 28
BibleProject ilibuni Tafakari ya Ujio wa Yesu ili kuhamasisha watu mmoja mmoja, vikundi vidogo vidogo, na familia kusherehekea majilio, au kuwasili kwa Yesu. Mwongozo huu wa wiki nne unashirikisha video za kikatuni, mihutasari mifupi, na maswali ya kutafakari ili kuwasaidia washiriki kuchunguza maana ya Biblia ya tumaini, amani, furaha, na upendo. Chagua mwongozo huu ili kujifunza jinsi maadili haya manne yamefika ulimwenguni kupitia kwa Yesu.
