“Mimi, Mwenyezi Mungu, nimekuita katika haki;
nitakushika mkono wako.
Nitakulinda na kukufanya kuwa agano
kwa ajili ya watu
na nuru kwa Mataifa,
kuwafungua macho wale wasioona,
kuwaacha huru kutoka kifungoni wale waliofungwa,
na kuwafungua kutoka gerezani
wale wanaokaa gizani.