1 Timotheo 6:1-2
1 Timotheo 6:1-2 NENO
Wale wote walio chini ya nira ya utumwa inawapasa kuwahesabu mabwana zao kuwa wanastahili heshima yote, ili jina la Mungu lisitukanwe wala mafundisho yetu. Wale watumwa ambao wana mabwana waaminio, haiwapasi kupunguza heshima yao kwa sababu wao ni ndugu. Badala yake, wawatumikie hata vizuri zaidi, kwa sababu wale wanaonufaika na huduma yao ni waumini, ambao ni wapendwa wao. Fundisha mambo haya na uwahimize kuyafuata.