Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 11

11
Zaburi 11
Kumtumaini Bwana
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1 Kwa Bwana ninakimbilia,
unawezaje basi kuniambia:
“Ruka kama ndege kwenye mlima wako.
2 Hebu tazama, waovu wanapinda pinde zao,
huweka mishale kwenye uzi wake,
wakiwa gizani ili kuwapiga
wale wanyofu wa moyo.
3 Wakati misingi imeharibiwa,
mwenye haki anaweza kufanya nini?”
4 Bwana yuko ndani ya Hekalu lake takatifu;
Bwana yuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni.
Huwaangalia wana wa watu,
macho yake yanawajaribu.
5 Bwana huwajaribu wenye haki,
lakini waovu na wanaopenda jeuri,
nafsi yake huwachukia.
6 Atawanyeshea waovu makaa ya moto mkali
na kiberiti kinachowaka,
upepo wenye joto kali ndio fungu lao.
7 Kwa kuwa Bwana ni mwenye haki,
yeye hupenda haki.
Wanyofu watauona uso wake.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 11: NEN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia