Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 123

123
Zaburi 123
Kuomba Rehema
Wimbo wa kwenda juu.
1 Ninayainua macho yangu kwako,
kwako wewe ambaye kiti chako cha enzi kiko mbinguni.
2 Kama vile macho ya watumwa
yatazamavyo mkono wa bwana wao,
kama vile macho ya mtumishi wa kike
yatazamavyo mkono wa bibi yake,
ndivyo macho yetu yamtazamavyo Bwana Mungu wetu,
mpaka atakapotuhurumia.
3Uturehemu, Ee Bwana, uturehemu,
kwa maana tumevumilia dharau nyingi.
4Tumevumilia dhihaka nyingi kutoka kwa wenye kiburi,
dharau nyingi kutoka kwa wenye majivuno.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 123: NEN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia