Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 28

28
Zaburi 28
Kuomba Msaada
Zaburi ya Daudi.
1 Ninakuita wewe, Ee Bwana, Mwamba wangu;
usiwe kwangu kama kiziwi.
Kwa sababu ukinyamaza
nitafanana na walioshuka shimoni.
2 Sikia kilio changu unihurumie
ninapokuita kwa ajili ya msaada,
niinuapo mikono yangu kuelekea
Patakatifu pa Patakatifu pako.
3 Usiniburute pamoja na waovu,
pamoja na hao watendao mabaya,
ambao huzungumza na jirani zao maneno mazuri,
lakini mioyoni mwao wameficha chuki.
4 Walipe sawasawa na matendo yao,
sawasawa na matendo yao maovu;
walipe sawasawa na kazi za mikono yao,
uwalipe wanavyostahili.
5 Kwa kuwa hawaheshimu kazi za Bwana,
na yale ambayo mikono yake imetenda,
atawabomoa na kamwe
hatawajenga tena.
6 Bwana asifiwe,
kwa maana amesikia kilio changu
nikimwomba anihurumie.
7 Bwana ni nguvu zangu na ngao yangu,
moyo wangu umemtumaini yeye,
nami nimesaidiwa.
Moyo wangu unarukaruka kwa furaha
nami nitamshukuru kwa wimbo.
8 Bwana ni nguvu ya watu wake,
ngome ya wokovu kwa mpakwa mafuta wake.
9 Waokoe watu wako na uubariki urithi wako;
uwe mchungaji wao na uwabebe milele.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 28: NEN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia