Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 61

61
Zaburi 61
Kuomba Ulinzi
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za uimbaji. Zaburi ya Daudi.
1 Ee Mungu, sikia kilio changu,
usikilize maombi yangu.
2 Kutoka miisho ya dunia ninakuita,
ninaita huku moyo wangu unadhoofika;
uniongoze kwenye mwamba
ule ulio juu kuliko mimi.
3 Kwa kuwa umekuwa kimbilio langu,
ngome imara dhidi ya adui.
4 Natamani kukaa hemani mwako milele,
na kukimbilia chini ya uvuli wa mbawa zako.
5 Ee Mungu, kwa kuwa umesikia nadhiri zangu,
umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.
6 Mwongezee mfalme siku za maisha yake,
miaka yake kwa vizazi vingi.
7 Yeye na atawazwe kwenye kiti cha enzi mbele za Mungu milele;
amuru upendo wako na uaminifu wako vimlinde.
8 Ndipo daima nitaliimbia sifa jina lako
na kuzitimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 61: NEN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia