Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 65

65
Zaburi 65
Kusifu Na Kushukuru
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo.
1 Ee Mungu, sifa zakungojea katika Sayuni;
kwako wewe nadhiri zetu zitatimizwa.
2 Ewe usikiaye maombi,
kwako wewe watu wote watakuja.
3 Tulipokuwa tumefunikwa kabisa na dhambi,
wewe ulisamehe makosa yetu.
4 Heri wale uliowachagua
na kuwaleta karibu ili waishi katika nyua zako!
Tunashibishwa kwa mema ya nyumba yako,
mema ya Hekalu lako takatifu.
5 Unatujibu kwa matendo ya kushangaza ya haki,
Ee Mungu Mwokozi wetu,
tumaini la miisho yote ya duniani
na la bahari zilizo mbali sana,
6 uliyeumba milima kwa uwezo wako,
ukiwa umejivika nguvu,
7 uliyenyamazisha dhoruba za bahari,
ngurumo za mawimbi yake,
na ghasia za mataifa.
8 Wale wanaoishi mbali sana
wanaogopa maajabu yako,
kule asubuhi ipambazukiapo
na kule jioni inakofifilia
umeziita nyimbo za furaha.
9 Waitunza nchi na kuinyeshea,
waitajirisha kwa wingi.
Vijito vya Mungu vimejaa maji
ili kuwapa watu nafaka,
kwa maana wewe umeviamuru.
10 Umeilowesha mifereji yake
na kusawazisha kingo zake;
umeilainisha kwa manyunyu
na kuibariki mimea yake.
11 Umeuvika mwaka taji ya baraka,
magari yako yanafurika kwa wingi.
12 Mbuga za majani za jangwani umezineemesha;
vilima vimevikwa furaha.
13 Penye nyanda za malisho pamejaa makundi ya wanyama,
na mabonde yamepambwa kwa mavuno;
vyote vinashangilia kwa furaha na kuimba.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 65: NEN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia