Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 84

84
Zaburi 84
Kuionea shauku nyumba ya Mwenyezi Mungu
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya wana wa Kora.
1Ee Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni,
makao yako yapendeza kama nini!
2Nafsi yangu inatamani sana,
naam, hata kuona shauku,
kwa ajili ya nyua za Mwenyezi Mungu;
moyo wangu na mwili wangu
vinamlilia Mungu Aliye Hai.
3Hata shomoro amejipatia makao,
mbayuwayu amejipatia kiota
mahali awezapo kuweka makinda yake:
mahali karibu na madhabahu yako,
Ee Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni,
Mfalme wangu na Mungu wangu.
4Heri wale wanaokaa nyumbani mwako,
wanaokusifu wewe daima.
5Heri wale ambao nguvu zao ziko kwako,
na njia ziendazo Sayuni zimo mioyoni mwao.
6Wanapopita katika Bonde la Baka#84:6 maana yake Bonde la Vilio,
hulifanya mahali pa chemchemi,
pia mvua za vuli hulijaza kwa madimbwi#84:6 au baraka.
7Huendelea toka nguvu hadi nguvu,
hadi kila mmoja afikapo
mbele za Mungu huko Sayuni.
8Ee Bwana Mwenyezi Mungu,
Mungu wa majeshi ya mbinguni,
sikia maombi yangu;
nisikilize, Ee Mungu wa Yakobo.
9Ee Mungu, uitazame ngao yetu,
mtazame kwa wema mpakwa mafuta wako.
10Siku moja katika nyua zako ni bora
kuliko siku elfu mahali pengine;
afadhali ningekuwa bawabu katika nyumba ya Mungu wangu
kuliko kukaa katika mahema ya waovu.
11Kwa kuwa Bwana Mwenyezi Mungu ni jua na ngao;
Mwenyezi Mungu hutoa wema na heshima;
hakuna kitu chema anachowanyima
wale ambao hawana hatia.
12Ee Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni,
heri mtu anayekutumaini wewe.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 84: NENO

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia