Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Tito Utangulizi

Utangulizi
Tito, kama vile Timotheo, alikuwa mshirika na rafiki wa karibu wa Paulo katika huduma yake. Alikuwa muumini asiyetahiriwa, mtu wa Mataifa kutoka Antiokia. Kama alifuatana na Paulo na Barnaba kuhudhuria baraza la Yerusalemu. Paulo alimwandikia Tito waraka huu muda mfupi tu baada ya kumwachia wajibu wa kuliangalia na kuliimarisha kanisa la Krete. Tito alikuwa na wajibu wa kuwateua wazee wa kanisa, kuwaweka wakfu, na kuwafundisha kushika misingi ya imani ya Kikristo.
Waraka huu unaonyesha kuwa kanisa la Krete halikuwa na mpangilio mahsusi. Ilimbidi Paulo aeleze kwa kina kuhusu sifa za wazee wa kanisa, na pia kutoa mafundisho kwa waumini. Paulo aligusia juu ya matatizo yanayowapata watumishi wa Mungu, na jinsi matatizo hayo yanavyoweza kutatuliwa.
Mwandishi
Mtume Paulo.
Kusudi
Kumshauri Tito kuhusu wajibu wake wa uangalizi wa makanisa katika kisiwa cha Krete.
Mahali
Pengine ni Korintho.
Tarehe
Mwaka wa 64 B.K.
Wahusika Wakuu
Paulo na Tito.
Wazo Kuu
Ingawa katika maisha yetu hapa duniani tumezungukwa na uovu na chuki, hatuna budi maisha yetu kuwa kielelezo jinsi neema ya Mungu inatupatia ushindi.
Mambo Muhimu
Kuweka mpango na uangalizi wa makanisa, na jinsi ya kufanya kazi hiyo. Mkazo wa barua hii ni kuhusu kuishi maisha matakatifu katika Kristo katikati ya uovu ulioko duniani. Paulo anarudia mara kwa mara kusisitiza kudumisha matendo mema.
Mgawanyo
Salamu (1:1-4)
Sifa za wazee wa kanisa (1:5-16)
Maelezo ya jumla kuhusu waumini (2:1-15)
Maagizo kuhusu maisha yawapasayo Wakristo (3:1-15).

Iliyochaguliwa sasa

Tito Utangulizi: NEN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia