Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zekaria 14:16-21

Zekaria 14:16-21 NEN

Kisha walionusurika katika mataifa yote ambayo yaliushambulia Yerusalemu watakuwa wakipanda Yerusalemu kila mwaka kumwabudu Mfalme, BWANA Mwenye Nguvu Zote na kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda. Ikiwa taifa lolote la dunia hawatakwenda Yerusalemu kumwabudu Mfalme, BWANA Mwenye Nguvu Zote, mvua haitanyesha kwao. Ikiwa watu wa Misri nao hawatakwenda kushiriki, hawatapata mvua. BWANA ataleta juu yao tauni ile ambayo itawapiga mataifa yale ambayo hayatakwenda kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda. Hii itakuwa adhabu ya Misri na adhabu ya mataifa yote yale ambayo hayatakwenda Yerusalemu kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda. Katika siku hiyo, kengele zilizofungwa kwenye farasi zitaandikwa maneno haya: TAKATIFU KWA BWANA, navyo vyungu vya kupikia katika nyumba ya BWANA vitakuwa kama bakuli takatifu mbele ya madhabahu. Kila chungu kilichoko Yerusalemu na Yuda kitakuwa kitakatifu kwa BWANA Mwenye Nguvu Zote na wote wanaokuja kutoa dhabihu watachukua baadhi ya vyungu hivyo na kupikia. Katika siku hiyo hatakuwepo tena mfanyabiashara katika nyumba ya BWANA Mwenye Nguvu Zote.

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zekaria 14:16-21