Zab 24
24
Kuingia Hekaluni
Ya Daudi. Zaburi.
1 #
1 Kor 10:26; Kut 9:29; Ayu 41:11 Nchi na vyote viijazavyo ni mali ya BWANA,
Dunia na wote wakaao ndani yake.
2Maana ameiweka misingi yake juu ya bahari,
Na juu ya mito ya maji aliithibitisha.
3Ni nani atakayepanda katika mlima wa BWANA?
Ni nani atakayesimama katika patakatifu pake?
4 #
Mt 5:8
Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe,
Asiyeiinua nafsi yake kwa ubatili,
Wala hakuapa kwa hila.
5Atapokea baraka kwa BWANA,
Na haki kwa Mungu wa wokovu wake.
6Hiki ndicho kizazi cha wamtafutao,
Wakutafutao uso wako, Ee Mungu wa Yakobo.
7 #
Hag 2:7; Mal 3:1; 1 Kor 2:8 Inueni vichwa vyenu, enyi malango,
Inukeni, enyi malango ya milele,
Mfalme wa utukufu apate kuingia.
8Ni nani Mfalme wa utukufu?
BWANA mwenye nguvu, hodari,
BWANA hodari wa vita.
9Inueni vichwa vyenu, enyi malango,
Naam, viinueni, enyi malango ya milele,
Mfalme wa utukufu apate kuingia.
10Ni nani huyu Mfalme wa utukufu?
BWANA wa majeshi,
Yeye ndiye Mfalme wa utukufu.
Iliyochaguliwa sasa
Zab 24: SUV
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
![None](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapistaging.com%2F58%2Fhttps%3A%2F%2Fweb-assets.youversion.com%2Fapp-icons%2Fsw.png&w=128&q=75)
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.