Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 43

43
Sala kwa Mungu Wakati wa Shida
1 # Zab 7:8 Ee Bwana, unihukumu, unitetee kwa taifa lisilo haki,
Uniokoe na mtu wa hila asiye haki.
2 # Zab 28:7; Isa 26:4 Kwa kuwa Wewe ndiwe Mungu uliye nguvu zangu; kwa nini umenitupa?
Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea?
3 # Zab 2:6; 3:4 Niletewe nuru yako na kweli yako ziniongoze,
Zinifikishe kwenye mlima wako mtakatifu na hata maskani yako.
4Hivyo nitakwenda madhabahuni kwa Mungu, kwa Mungu aliye
furaha yangu na shangwe yangu;
Nitakusifu kwa kinubi, Ee MUNGU, Mungu wangu.
5 # Zab 42:5,11 Nafsi yangu, kwa nini kuinama,
Na kufadhaika ndani yangu?
Umtumaini Mungu;
Kwa maana nitakuja kumsifu,
Aliye afya ya uso wangu,
Na Mungu wangu.

Iliyochaguliwa sasa

Zab 43: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia