Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Ezekieli 43

43
Utukufu wa Mungu warudi hekaluni
1 # Eze 10:19 Kisha akanileta mpaka langoni, yaani, lango lile lielekealo upande wa mashariki; 2#Isa 6:3; Eze 3:23; 9:3; 10:3-4,18-19; 11:22-23; Ufu 1:15; 18:1 na tazama, huo utukufu wa Mungu wa Israeli ulitokea kwa njia ya mashariki; na sauti yake ilikuwa kama mshindo wa maji mengi, nayo nchi iling'aa kwa utukufu wake. 3#Eze 1:4; 3:23; Yer 1:10 Na maono niliyoyaona yalikuwa kama maono niliyoyaona nilipokuja kuuharibu mji; nayo maono niliyoyaona yalikuwa kama maono niliyoyaona karibu na mto wa Kebari; nikaanguka kifudifudi. 4#Eze 10:19 Na huo utukufu wa BWANA ukaingia ndani ya nyumba, kwa njia ya lango lile lielekealo upande wa mashariki. 5#Eze 3:12; 1 Fal 8:10 Kisha Roho ikaniinua, ikanichukua mpaka katika ua wa ndani; na tazama, utukufu wa BWANA uliijaza nyumba. 6#Eze 40:3 Nikasikia sauti ya mmoja asemaye nami, itokayo katika nyumba hiyo; na mtu akasimama karibu nami. 7#Zab 99:1,5; 68:16; 1 Nya 28:2; Kut 25:8; Law 26:12,30; Eze 39:7; Yer 16:18 Akaniambia, Mwanadamu, hapa ni mahali pa kiti changu cha enzi, na mahali pa nyayo za miguu yangu, nitakapokaa kati ya wana wa Israeli milele; na nyumba ya Israeli hawatalinajisi jina langu takatifu tena, wao, wala wafalme wao, kwa mambo yao ya kikahaba, na kwa mizoga ya wafalme wao, katika mahali pao pa juu; 8#2 Fal 16:14 kwa kuweka kizingiti chao karibu na kizingiti changu; na mwimo wao karibu na mwimo wangu; tena palikuwa na ukuta tu kati ya mimi na wao; nao wamelinajisi jina langu takatifu kwa machukizo yao waliyoyatenda; basi, kwa sababu hiyo, nimewaangamiza katika hasira yangu. 9Basi sasa wayaondoe mambo yao ya kikahaba, na mizoga ya wafalme wao, yawe mbali nami, nami nitakaa kati yao milele.
10 # Eze 40:4 Na wewe, mwanadamu, waoneshe wana wa Israeli nyumba hii, ili wayatahayarikie maovu yao; na waipime hesabu yake. 11#Eze 44:5,6; Mt 28:20 Na ikiwa wameyatahayarikia yote waliyoyatenda, waoneshe umbo la nyumba, na namna yake, na matokeo yake, na maingilio yake, na maumbo yake yote, na maagizo yake yote, na kawaida zake zote, na sheria zake zote, ukayaandike machoni pao; ili walishike umbo lake lote, na maagizo yake, na kuyatenda. 12#Zab 93:5; Eze 40:2; Ufu 21:27 Hii ndiyo sheria ya nyumba; juu ya kilele cha mlima, mpaka wake wote pande zote patakuwa patakatifu sana. Tazama, hii ndiyo sheria ya nyumba.
Madhabahu
13 # Eze 40:5; Kut 27:1-2; 2 Nya 4:1 Na vipimo vya madhabahu kwa dhiraa ni hivi; (dhiraa ni dhiraa na shubiri); kitako chake ni dhiraa moja, na upana wake dhiraa moja; na pambizo yake karibu na ncha yake pande zote, shubiri moja; na hiki kitakuwa kitako cha madhabahu. 14Tena toka chini, juu ya nchi, hadi daraja ya chini, dhiraa mbili, na upana wake dhiraa moja; tena toka daraja ndogo hadi daraja kubwa, dhiraa nne, na upana wake dhiraa moja. 15Na madhabahu ya juu itakuwa dhiraa nne; na toka madhabahu pawashwapo moto na kwenda juu zitakuwa pembe nne. 16Na pale pawashiwapo moto, urefu wake dhiraa kumi na mbili, na upana wake kumi na mbili, mraba pande zake nne. 17#Kut 20:26 Na daraja, urefu wake dhiraa kumi na nne, na upana wake dhiraa kumi na nne, pande zake nne; na pambizo yake nusu dhiraa; na kitako chake dhiraa moja, kotekote, na madaraja yake yataelekea upande wa mashariki.
18 # Law 1:5; Ebr 9:18-22; Kut 29:35-37 Kisha akaniambia, Mwanadamu, Bwana MUNGU asema hivi; Hizi ndizo sheria za madhabahu katika siku ile watakapoifanya, ili watoe sadaka za kuteketezwa juu yake, na kunyunyiza damu juu yake. 19#1 Fal 2:27,35; Isa 61:5; Yer 33:18; Eze 40:46; Kut 29:10; Law 8:14,15 Utawapa makuhani Walawi, walio wa uzao wa Sadoki, walio karibu nami, ili kunihudumu, asema Bwana MUNGU, ng'ombe dume mchanga awe sadaka ya dhambi. 20Nawe utatwaa baadhi ya damu yake, na kuitia juu ya pembe zake nne, na juu ya ncha nne za daraja, na juu ya pambizo yake pande zote; ndivyo utakavyoitakasa, na kuifanyia upatanisho. 21#Kut 29:14; Ebr 13:11 Tena utamtwaa ng'ombe wa sadaka ya dhambi, naye utamteketeza mahali palipoamriwa pa nyumba ile, nje ya mahali patakatifu. 22Na siku ya pili utamtoa beberu mkamilifu awe sadaka ya dhambi; nao wataisafisha madhabahu, kama walivyoisafisha kwa ng'ombe huyo. 23Utakapokwisha kuitakasa, utatoa ng'ombe dume mchanga mkamilifu, na kondoo dume wa kundini mkamilifu. 24#Law 2:13 Nawe utawaleta karibu mbele za BWANA, na makuhani watamwaga chumvi juu yao, nao watawatoa wawe sadaka za kuteketezwa kwa BWANA. 25#Kut 29:35 Kwa muda wa siku saba utaandaa mbuzi kila siku awe sadaka ya dhambi; pia wataandaa ng'ombe dume mchanga, na kondoo dume wa kundini, wakamilifu. 26Kwa muda wa siku saba wataifanyia madhabahu upatanisho, na kuitakasa; ndivyo watakavyoiweka wakfu. 27#Law 9:1; Ayu 42:8 Nao watakapozitimiza siku hizo, itakuwa, siku ya nane na baadaye, makuhani watatoa sadaka zenu za kuteketezwa juu ya madhabahu, na sadaka zenu za amani nami nitawakubali ninyi, asema Bwana MUNGU.

Iliyochaguliwa sasa

Ezekieli 43: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia