Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Isaya 51

51
Baraka walizowekewa watu wa Mungu
1 # Mit 15:9; Mt 6:33; Rum 9:30 Nisikilizeni, ninyi mnaoifuatia haki; ninyi mnaomtafuta BWANA; uangalieni mwamba ule ambao mlitolewa kwa kuchongwa, na tundu la shimo ambalo mlitolewa kwa kuchimbuliwa. 2#Rum 4:1; Ebr 11:11 Mwangalieni Abrahamu, baba yenu, na Sara, aliyewazaa; kwa maana alipokuwa mmoja tu nilimwita, nikambariki, nikamfanya kuwa wengi. 3#Zab 102:13; Isa 40:1; Mwa 13:10; Yoe 2:3 Maana BWANA ameufariji Sayuni; amepafariji mahali pake palipokuwa ukiwa; amefanya nyika yake kuwa kama bustani ya Edeni, na jangwa lake kama bustani ya BWANA; shangwe na furaha zitaonekana ndani yake, kushukuru, na sauti ya kuimba.
4Nisikilizeni mimi, enyi watu wangu; nisikieni, taifa langu; maana sheria itatoka kwangu, na kutoa haki yangu iwe nuru ya mataifa. 5#Isa 46:13; Rum 1:16 Haki yangu i karibu, wokovu wangu umekuwa wazi, na mikono yangu itawahukumu makabila ya watu; visiwa vitaningoja, navyo vitautumainia mkono wangu. 6#Mt 24:35; 2 Pet 3:10 Inueni macho yenu mbinguni, mkaitazame nchi chini; maana mbingu zitatoweka kama moshi, na nchi itachakaa kama vazi, nao wakaao ndani yake watakufa kadhalika; bali wokovu wangu utakuwa wa milele, na ukombozi wangu hautakoma kamwe.
7 # Zab 37:31; Mt 10:28; Lk 12:4; Mdo 5:41 Nisikilizeni, ninyi mjuao haki, watu ambao mioyoni mwenu mna sheria yangu; msiogope masuto ya watu, wala msifadhaike kwa sababu ya dhihaka zao. 8Maana nondo atawala kama vazi, na funza atawala kama sufu; bali haki yangu itakuwa ya milele, na wokovu wangu hata vizazi vyote.
9 # Ufu 11:17; Ayu 26:12; Zab 87:4; Eze 29:3 Amka, amka, jivike nguvu,
Ee mkono wa Bwana;
Amka kama katika siku zile za kale,
Katika vizazi vile vya zamani.
10 # Kut 14:21 Si wewe uliyemkatakata Rahabu?
Uliyemchoma yule joka?
Si wewe uliyeikausha bahari,
Na maji ya vilindi vikuu;
Uliyevifanya vilindi kuwa njia,
Ili wapite watu waliokombolewa?
11Nao waliokombolewa na BWANA watarejea,
Watafika Sayuni, wakiimba;
Furaha ya milele itakuwa juu ya vichwa vyao;
Watapata shangwe na furaha;
Huzuni na kuugua zitakimbia.
12 # 2 Kor 1:3; Zab 118:6; 1 Pet 1:24 Mimi, naam, mimi, ndimi niwafarijiye; wewe u nani hata ukamwogopa mtu atakayekufa, na mwanadamu atakayefanywa kuwa kama majani? 13#Ayu 9:8; 20:7 Ukamsahau BWANA, Muumba wako, yeye aliyezitanda mbingu, na kuiweka misingi ya dunia; nawe unaogopa daima mchana kutwa kwa sababu ya ghadhabu yake yeye aoneaye, hapo ajitayarishapo kuharibu; nayo i wapi ghadhabu yake aoneaye? 14#Zek 9:11 Yeye aliyehamishwa na kufungwa atafunguliwa kwa haraka; wala hatakufa na kushuka shimoni, wala chakula chake hakitapunguka. 15#Kut 14:21; Zab 74:13; 93:3,4; Isa 17:12; 43:16 Maana mimi ni BWANA, Mungu wako, niichafuaye bahari, mawimbi yake yakavuma. 16#Kum 18:18; Yn 3:34; Isa 59:21; 65:17; 2 Pet 3:13 BWANA wa majeshi ndilo jina lake. Nami nimetia maneno yangu kinywani mwako, nami nimekusitiri katika kivuli cha mkono wangu, ili nizipande mbingu, na kuiweka misingi ya dunia, na kuuambia Sayuni, Ninyi ni watu wangu.
17 # Kum 28:28,34; Zab 60:3; Ufu 14:10; 16:19 Amka, amka, simama, Ee Yerusalemu,
Wewe uliyenywea mkononi mwa BWANA,
Kikombe cha hasira yake;
Ukalinywea na kumaliza bakuli la kulevyalevya
Umelinywea na kulimaliza.
18Hapana hata mmoja wa kumwongoza
Miongoni mwa wana wote aliowazaa,
Wala hapana hata mmoja wa kumshika mkono
Miongoni mwa wana wote aliowalea.
19 # Amo 7:2 Mambo haya mawili yamekupata;
Ni nani awezaye kukusikitikia?
Ukiwa na uharibifu, na njaa na upanga;
Niwezeje kukutuliza?
20 # Omb 2:11,12 Wana wako wamezimia,
Wamelala penye pembe za njia kuu zote
Kama kulungu wavuni;
Wamejaa hasira ya BWANA,
Lawama ya Mungu wako.
21Basi, kwa sababu ya hayo, ulisikilize neno hili, ewe uliyeteswa, na kulewa, lakini si kwa mvinyo; 22#Yer 50:34 BWANA, Bwana wako na Mungu wako, awateteaye watu wake, asema hivi, Tazama, nimeondoa mkononi mwako kikombe cha kulevyalevya, hilo bakuli la hasira yangu; hutalinywea tena; 23#Zek 12:2; Zab 66:11,12 nami nitalitia mikononi mwao wakutesao; waliokuambia nafsi yako, Inama, tupate kupita; nawe uliufanya mgongo wako kuwa kama nchi, na kama njia, kwa hao wapitao juu yake.

Iliyochaguliwa sasa

Isaya 51: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia