Zaburi 128
128
Nyumba ya mwumini yenye furaha
Wimbo wa kupanda mlima.
1Heri kila mtu amchaye BWANA,
Aendaye katika njia yake.
2 #
Isa 3:10
Taabu ya mikono yako hakika utaila;
Utakuwa heri, na kwako kwema.
3Mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao,
Katika nyumba yako.
Wanao watakuwa kama miche ya mizeituni
Wakiizunguka meza yako.
4Tazama, atabarikiwa hivyo, yule amchaye BWANA.
5 #
Zab 134:3
BWANA akubariki toka Sayuni;
Uone uheri wa Yerusalemu siku zote za maisha yako;
6 #
Mwa 50:23
Naam, ukawaone wana wa wanao.
Amani ikae na Israeli.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 128: SRUV
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Zaburi 128
128
Nyumba ya mwumini yenye furaha
Wimbo wa kupanda mlima.
1Heri kila mtu amchaye BWANA,
Aendaye katika njia yake.
2 #
Isa 3:10
Taabu ya mikono yako hakika utaila;
Utakuwa heri, na kwako kwema.
3Mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao,
Katika nyumba yako.
Wanao watakuwa kama miche ya mizeituni
Wakiizunguka meza yako.
4Tazama, atabarikiwa hivyo, yule amchaye BWANA.
5 #
Zab 134:3
BWANA akubariki toka Sayuni;
Uone uheri wa Yerusalemu siku zote za maisha yako;
6 #
Mwa 50:23
Naam, ukawaone wana wa wanao.
Amani ikae na Israeli.
Iliyochaguliwa sasa
:
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.