Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 57

57
Sifa na hakikisho katika mateso
Kwa mwimbishaji: kwa mtindo wa Usiharibu. Utenzi wa Daudi alipomponyoka Sauli na kujificha pangoni.
1 # Isa 26:20 Unirehemu, Ee Mungu, unirehemu mimi,
Maana nafsi yangu imekukimbilia Wewe.
Nitaukimbilia uvuli wa mbawa zako,
Hadi misiba hii itakapopita.
2 # Zab 138:8 Nitamwita MUNGU Aliye Juu,
Mungu anitimiziaye mambo yangu.
3 # Zab 144:5; 40:11 Atanitumia msaada toka mbinguni na kuniokoa,
Atawaaibisha wale wanaotaka kunishambulia.
Mungu atazituma
Fadhili zake na kweli yake.
4 # Mit 30:14; Zab 64:3 Nafsi yangu i kati ya simba,
Nitastarehe kati yao waliowaka moto.
Wanadamu meno yao ni mikuki na mishale,
Na ndimi zao ni upanga mkali.
5 # Zab 108:5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu,
Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako.
6 # Zab 9:15 Wameweka wavu ili kuninasa miguu;
Nimevunjika moyo;
Wamechimba shimo njiani mwangu;
Lakini wao wenyewe wametumbukia humo!
7 # Zab 108:1 Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti,
Moyo wangu ni thabiti.
Nitaimba, nitaimba kwa sauti nzuri,
8 # Amu 5:12 Amka, ee moyo wangu.
Amka, kinanda na kinubi,
Nitaamka alfajiri.
9Ee Bwana, nitakushukuru kati ya watu,
Nitakuimbia sifa kati ya mataifa.
10 # Zab 108:4 Maana fadhili zako ni kubwa hata mbinguni,
Na uaminifu wako hata mawinguni.
11Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu,
Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 57: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia