Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 8

8
Utukufu wa Mungu na hadhi ya utu
Kwa mwimbishaji: kwa kufuata Gitithi. Zaburi ya Daudi.
1Ee, MUNGU, Bwana wetu
Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani kote!
Wewe umeuweka utukufu wako mbinguni;
2 # Mt 21:16; 11:25; 1 Kor 1:27 Vinywani mwa watoto wachanga na wanyonyao
Umeiweka misingi ya nguvu;
Kwa sababu yao wanaoshindana nawe;
Uwakomeshe adui na mjilipiza kisasi.
3 # Zab 44:16; 19:1; Ayu 22:12; Rum 1:20 Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako,
Mwezi na nyota ulizoziratibisha;
4 # Ayu 7:17-18; Zab 144:3; Ebr 2:6-8 Mtu ni kitu gani hata umkumbuke,
Na binadamu hata umwangalie?
5Umemfanya mdogo kuliko Mungu;
Umemvika taji la utukufu na heshima;
6 # 1 Kor 15:27; Efe 1:22; Ebr 2:8; Mwa 1:26 Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako;
Umevitia vitu vyote chini ya miguu yake.
7Kondoo, na ng'ombe wote pia;
Naam, na wanyama wa porini;
8Ndege wa angani, na samaki wa baharini;
Na kila kipitacho njia za baharini.
9 # Ayu 11:7; Zab 35:10 Wewe, MUNGU, Bwana wetu,
Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani kote!

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 8: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia