Nehemia UTANGULIZI
UTANGULIZI
Kitabu hiki kinaendeleza masimulizi ya kitabu kilichotangulia, yaani Kitabu cha Ezra. Nehemia aliishi wakati wa Ezra na alikuwa Afisa maarufu katika utawala wa Artashasta, mfalme wa Persia. Nehemia alipata kibali kutoka kwa mkuu wake arudi Yerusalemu ajishughulishe na urekebishaji wa maisha ya siasa, uchumi na jamii (sura 1:1–2:10). Mara alipowasili huko, ingawa alikumbana na upinzani kutoka kwa maadui fulani, aliungwa mkono na baadhi ya wananchi wenzake wakajenga kuta za mji wa Yerusalemu (sura 2:11–7:72). Nehemia na Ezra walikuwako wakati wa mkutano mkubwa wa kidini ambamo Ezra alihutubu juu ya sheria ya Mungu.
Watu walirudia tena maagano yao kwa Mungu (sura 8:1–10:40). Baada ya kutoa mawaidha mbalimbali yaliyohusu hasa mambo ya siasa, Nehemia alisimamia kuwekwa wakfu kwa kuta zilizojengwa upya (11:11–12:43), kisha akaendelea na mambo mengine ya kurekebisha mfumo wa dini (sura 12:44–13:31).
Iliyochaguliwa sasa
Nehemia UTANGULIZI: BHN
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Nehemia UTANGULIZI
UTANGULIZI
Kitabu hiki kinaendeleza masimulizi ya kitabu kilichotangulia, yaani Kitabu cha Ezra. Nehemia aliishi wakati wa Ezra na alikuwa Afisa maarufu katika utawala wa Artashasta, mfalme wa Persia. Nehemia alipata kibali kutoka kwa mkuu wake arudi Yerusalemu ajishughulishe na urekebishaji wa maisha ya siasa, uchumi na jamii (sura 1:1–2:10). Mara alipowasili huko, ingawa alikumbana na upinzani kutoka kwa maadui fulani, aliungwa mkono na baadhi ya wananchi wenzake wakajenga kuta za mji wa Yerusalemu (sura 2:11–7:72). Nehemia na Ezra walikuwako wakati wa mkutano mkubwa wa kidini ambamo Ezra alihutubu juu ya sheria ya Mungu.
Watu walirudia tena maagano yao kwa Mungu (sura 8:1–10:40). Baada ya kutoa mawaidha mbalimbali yaliyohusu hasa mambo ya siasa, Nehemia alisimamia kuwekwa wakfu kwa kuta zilizojengwa upya (11:11–12:43), kisha akaendelea na mambo mengine ya kurekebisha mfumo wa dini (sura 12:44–13:31).
Iliyochaguliwa sasa
:
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.