Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 99

99
Mungu mtawala mkuu
1Mwenyezi-Mungu anatawala,
mataifa yanatetemeka!
Ameketi juu ya viumbe vyenye mabawa,#99:1 viumbe vyenye mabawa: Taz. maelezo ya Mwa. 3:24
nayo dunia inatikisika!
2Mwenyezi-Mungu ni mkuu katika Siyoni;
ametukuka juu ya mataifa yote.
3Wote na walisifu jina lake kuu la kutisha.
Mtakatifu ndiye yeye!
4Ee mfalme mkuu, mpenda uadilifu!
Umethibitisha haki katika Israeli;
umeleta uadilifu na haki.
5Msifuni Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu;
angukeni kifudifudi mbele zake.
Mtakatifu ndiye yeye!
6Mose na Aroni walikuwa makuhani wake;
Samueli alikuwa miongoni mwa waliomlilia.
Walimlilia Mwenyezi-Mungu naye akawasikiliza.
7Alisema nao katika mnara wa wingu;
waliyazingatia matakwa yake na amri alizowapa.
8Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, wewe uliwasikiliza;
kwao ulikuwa Mungu mwenye kusamehe,
ingawa uliwaadhibu kwa makosa yao.
9Msifuni Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu;
abuduni katika mlima wake mtakatifu!#99:9 mlima wake mtakatifu: Taz Zab 2:6.
Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, ni mtakatifu.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 99: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia