Hesabu 35:32 - Linganisha Matoleo Yote
Hesabu 35:32 BHN (Biblia Habari Njema)
Msipokee wala msikubali fidia yoyote kutoka kwa mtu aliyekimbilia mji wa makimbilio ili kumruhusu arudi kukaa nyumbani kwake kabla ya kifo cha kuhani mkuu.
Shirikisha
Hesabu 35 BHNHesabu 35:32 SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Tena hamtapokea fidia kwa ajili ya huyo aliyeukimbilia mji wake wa makimbilio, apate kwenda tena kuketi katika nchi, hata kifo cha kuhani mkuu.
Shirikisha
Hesabu 35 SUVHesabu 35:32 SRUV (Swahili Revised Union Version)
Tena hamtapokea fidia kwa ajili ya huyo aliyeukimbilia mji wake wa makimbilio, apate kwenda tena kukaa katika nchi, hata kifo cha kuhani mkuu.
Shirikisha
Hesabu 35 SRUVHesabu 35:32 NEN (Neno)
“ ‘Usikubali fidia ya mtu ambaye amekimbilia katika mji wa makimbilio, na hivyo kumruhusu kurudi kuishi katika nchi yake kabla ya kifo cha kuhani mkuu.
Shirikisha
Hesabu 35 NEN