Nao wale wanawake wakaitikiana wakicheza, wakasema,
Sauli amewaua elfu zake,
Na Daudi makumi elfu yake.
Basi Sauli akaghadhibika sana, na maneno haya yakamchukiza; akasema, Wamempa Daudi makumi elfu, na mimi wamenipa elfu tu; kuna nini tena awezayo kupata, isipokuwa ni ufalme?