YouVersion Logo
Search Icon

Habakuki Utangulizi

Utangulizi
Habakuki maana yake ni “Kumbatia.” Alikuwa nabii wa Yuda wa kabila la Lawi, mmoja wa waimbaji katika Hekalu. Kitabu hiki kimeandikwa kwa mtindo wa mazungumzo kati ya Mungu na nabii. Habakuki hakuelewa jinsi gani Mungu angeweza kuwatumia Wakaldayo, waliokuwa waovu kuliko Wayahudi, kutekeleza hukumu dhidi ya watu waliokuwa wamechaguliwa na Mungu. Jibu la Mungu lilikuwa kwamba wenye haki wangeishi kwa imani kwa Mungu, na kwamba walikuwa na uhakika kwamba Mungu alikuwa anafanya lililo sahihi. Mungu alimwambia Habakuki kwamba punde si punde Wakaldayo wangehukumiwa, na kwamba hatimaye haki ingeshinda kwa ajili ya watu wa Mungu.
Mwandishi
Habakuki.
Kusudi
Kuonyesha kwamba bado Mungu anaitawala dunia. Hata kama tunaona uovu ukishamiri, kuna siku Mungu atahukumu na kuadhibu huo uovu, na hatimaye kuuangamiza kabisa, usiwepo tena.
Mahali
Yuda.
Tarehe
Kati ya 612–589 K.K.
Wahusika Wakuu
Habakuki, na Wakaldayo.
Wazo Kuu
Mungu anaweza kuwatumia waovu kuadhibu watu wake wanapotenda dhambi kwa nia ya kuwarudisha kwake. Lakini hao waovu wakiisha kutimiza kusudi la Mungu, wao nao huadhibiwa zaidi.
Mambo Muhimu
Mungu hutumia watu waovu kuwaadhibu watu wake wanapokosea. Imani na mamlaka ya Mungu ni uhakika kwamba Mungu ana haki katika njia zake zote.
Mgawanyo
Swali la Habakuki na jibu la Mungu (1:1-11)
Swali la pili la Habakuki na jibu la Mungu (1:12–2:20)
Maombi ya Habakuki (3:1-19).

Currently Selected:

Habakuki Utangulizi: NEN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in