YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 1

1
KITABU CHA KWANZA
(Zaburi 1–41)
Zaburi 1
Furaha Ya Kweli
1 Heri mtu yule ambaye
haendi katika shauri la watu waovu,
wala hasimami katika njia ya wenye dhambi,
au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
2 Bali huifurahia sheria ya Bwana,
naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
3 Mtu huyo ni kama mti uliopandwa
kando ya vijito vya maji,
ambao huzaa matunda kwa majira yake
na majani yake hayanyauki.
Lolote afanyalo hufanikiwa.
Huzuni Ya Waovu
4 Sivyo walivyo waovu!
Wao ni kama makapi
yapeperushwayo na upepo.
5 Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu,
wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
6Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki,
bali njia ya waovu itaangamia.

Currently Selected:

Zaburi 1: NEN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

Video for Zaburi 1