YouVersion Logo
Search Icon

1 Wathesalonike 4

4
Maisha yampendezayo Mungu
1 # 2 The 3:6 Iliyobaki, ndugu, tunawasihi na kuwaonya kwamba mwenende katika Bwana Yesu; kama mlivyopokea kwetu jinsi iwapasavyo kuenenda na kumpendeza Mungu, kama nanyi mnavyoenenda, vivyo hivyo mpate kuzidi sana. 2Kwa kuwa mnajua ni maagizo gani tuliyowapa kwa Bwana Yesu. 3#1 The 5:23; Ebr 10:10; 1 Pet 1:16 Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati; 4#1 Kor 6:13,15 kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima; 5#Yer 10:25; Zab 79:6 si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu. 6#Zab 94:2 Mtu asimpunje ndugu yake wala kumkosea katika jambo hili; kwa sababu Bwana ndiye alipizaye kisasi cha haya yote; kama tulivyowaambia kwanza, tukashuhudia sana. 7#2 The 2:13,14 Maana Mungu hakutuitia uchafu, bali tuwe katika utakaso. 8#Lk 10:16; Eze 36:27; 37:14 Basi yeye anayekataa, hakatai mwanadamu bali Mungu, anayewapa ninyi Roho wake Mtakatifu.
9 # Yn 13:34; Yer 31:33,34 Kuhusu upendano, hamna haja niwaandikie; maana ninyi wenyewe mmefundishwa na Mungu kupendana. 10#2 The 3:4 Kwa maana mnafanya neno hili kwa ndugu wote walio katika Makedonia yote. Lakini tunawasihi, ndugu, mzidi sana. 11#Efe 4:28; 2 The 3:8,12 Tena mjitahidi kutulia, na kutenda shughuli zenu, na kufanya kazi kwa mikono yenu wenyewe, kama tulivyowaagiza; 12#Kol 4:5; 1 Kor 5:12,13 ili mwende kwa adabu mbele yao walio nje, wala msiwe na haja ya kitu chochote.
Kuja kwa Bwana
13 # 1 Kor 15:20; Efe 2:12 Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini. 14#Rum 14:9; 1 Kor 15:3,4,12 Maana, ikiwa tunaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye. 15#1 Kor 15:51-52; 7:10,25 Kwa kuwa tunawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti. 16#1 Kor 15:52; 2 The 1:7 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. 17#Yn 12:26; 17:24 Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele. 18Basi, farijianeni kwa maneno hayo.

Currently Selected:

1 Wathesalonike 4: SRUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

Video for 1 Wathesalonike 4