YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 4

4
Ombi la kuokolewa kutoka kwa adui
Kwa mwimbishaji: kwa ala za muziki zenye nyuzi. Zaburi ya Daudi.
1Ee Mungu wa haki yangu, uniitikie niitapo;
Uliniokoa nilipokuwa katika shida;
Unifadhili na kuisikia sala yangu.
2Enyi wanadamu, hadi lini utukufu wangu utafedheheka?
Je! Mtapenda ubatili na kutafuta uongo hadi lini?
3 # Kut 33:16; 2 Pet 2:9 Bali jueni ya kuwa BWANA amejiteulia mtauwa;
BWANA husikia nimwitapo.
4 # Efe 4:26; Mit 3:7 Muwe na hofu wala msitende dhambi,
Tafakarini vitandani mwenu na kutulia.
5 # Kum 33:19; Zab 37:3 Toeni dhabihu za haki,
Na kumtumaini BWANA.
6 # Zab 80:3 Wengi husema, Nani atakayetuonesha mema?
BWANA, utuinulie nuru ya uso wako.
7Umenitia furaha moyoni mwangu,
Kupita yao wanapozidishiwa nafaka na divai.
8 # Law 26:5; Kum 12:10; Yn 14:27; Flp 4:7 Katika amani nitajilaza na kupata usingizi mara,
Maana Wewe, BWANA, peke yako,
Ndiwe unijaliaye kukaa salama.

Currently Selected:

Zaburi 4: SRUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

Videos for Zaburi 4