YouVersion Logo
Search Icon

Malaki UTANGULIZI

UTANGULIZI
Kitabu cha Malaki huenda kiliandikwa mnamo sehemu ya kwanza ya karne ya 5 K.K., karibu miaka 100 baada ya Waisraeli kurudi nchini mwao kutoka uhamishoni Babuloni.
Miaka thelathini au hamsini kabla ya mahubiri ya Malaki, Waisraeli walikuwa wameitikia mwito wa manabii Hagai na Zekaria kujenga upya hekalu la Yerusalemu (520-515 K.K.). Lakini kidogo kidogo tazamio lao la hali mpya chini ya uongozi wa mtawala Zerubabeli lilianza kufifia. Hali ya kidini na maisha adili ilianza kufifia: Ibada kwa Mungu ikasahauliwa (1:6-14), makuhani wakazembea katika huduma yao, nayo sheria ya Mungu ikawa inapuuzwa (2:1-16). Hali hiyo ilimfanya nabii huyu Malaki kuwahimiza watu wafanye mabadiliko thabiti na ya kimsingi katika maisha yao kwa kuwakumbusha upendo wa Mungu (1:1-5) na pia kwamba adhabu yake iko karibu (2:17–3:5; 3:13–4:6). Aliwatangazia kwamba Mungu atamtuma mtumishi wake (3:10) ambaye atakuwa nabii kama Elia (4:5). Katika Injili – Agano Jipya, ahadi hiyo inaoneshwa kukamilika katika huduma ya Yohane Mbatizaji ambaye alikuwa na jukumu la kutayarisha ujio wa Yesu Kristo (Mat 17:11-13; Luka 1:17).

Currently Selected:

Malaki UTANGULIZI: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in