YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 137

137
Ombolezo ugenini
1Kando ya mito ya Babuloni, tulikaa,
tukawa tunalia tulipokumbuka Siyoni.
2Katika miti ya nchi ile,
tulitundika zeze zetu.
3Waliotuteka walitutaka tuwaimbie;
watesi wetu walitutaka tuwafurahishe:
“Tuimbieni mojawapo ya nyimbo za Siyoni!”
4Twawezaje kuimba wimbo wa Mwenyezi-Mungu
katika nchi ya kigeni?
5Ee Yerusalemu, kama nikikusahau,
mkono wangu wa kulia na ukauke!
6Ulimi wangu na uwe mzito,
kama nisipokukumbuka wewe, ee Yerusalemu;
naam, nisipokuthamini kuliko furaha yangu kubwa!
7Ee Mwenyezi-Mungu, usisahau waliyotenda Waedomu,
siku ile Yerusalemu ilipotekwa;
kumbuka waliyosema:
“Bomoeni mji wa Yerusalemu!
Ngoeni hata na misingi yake!”
8 # Taz Ufu 18:6 Ee Babuloni, utaangamizwa!
Heri yule atakayekulipiza mabaya uliyotutenda!
9Heri yule atakayewatwaa watoto wako
na kuwapondaponda mwambani!

Currently Selected:

Zaburi 137: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

Videos for Zaburi 137