1
Mwanzo 22:14
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
Kwa hiyo, Abrahamu akapaita pahali pale: “Yawe anajalia,” kama inavyosemwa hata leo: “Kwa mulima wa Yawe, watu wanajaliwa.”
Comparar
Explorar Mwanzo 22:14
2
Mwanzo 22:2
Mungu akamwambia: “Umutwae mwana wako, Isaka, mwana wako wa pekee unayemupenda, uende mpaka inchi ya Moria, umutoe kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto juu ya mulima nitakaokuonyesha.”
Explorar Mwanzo 22:2
3
Mwanzo 22:12
Malaika akamwambia: “Usinyooshe mukono wako juu ya kijana wala usimufanyie jambo lolote! Sasa ninajua kwamba unamwogopa Mungu, maana haukuninyima hata mwana wako wa pekee.”
Explorar Mwanzo 22:12
4
Mwanzo 22:8
Abrahamu akamujibu: “Mwana wangu, Mungu mwenyewe atatujalia mwana-kondoo wa sadaka ya kuteketezwa.” Basi, wakaendelea na safari yao.
Explorar Mwanzo 22:8
5
Mwanzo 22:17-18
hakika nitakubariki, na wazao wako nitawazidisha kama nyota mbinguni na kama muchanga pembeni ya bahari. Wazao wako watarizi miji ya waadui zao. Kutokana na wazao wako mataifa yote katika dunia yatabarikiwa kwa sababu wewe umeitii amri yangu.”
Explorar Mwanzo 22:17-18
6
Mwanzo 22:1
Nyuma ya mambo yale, Mungu alimupima Abrahamu. Mungu alimwita: “Abrahamu!” Naye akaitika: “Niko hapa.”
Explorar Mwanzo 22:1
7
Mwanzo 22:11
Lakini malaika wa Yawe akamwita kutoka mbinguni: “Abrahamu! Abrahamu!” Naye akaitika: “Niko hapa!”
Explorar Mwanzo 22:11
8
Mwanzo 22:15-16
Malaika wa Yawe akamwita Abrahamu mara ya pili kutoka mbinguni, akamwambia: “Yawe anasema hivi: Nimeapa kwa nafsi yangu mwenyewe kwamba kwa sababu umefanya hivi, wala haukuninyima mwana wako wa pekee
Explorar Mwanzo 22:15-16
9
Mwanzo 22:9
Walipofika pahali ambapo Mungu alipomwagiza, Abrahamu akajenga mazabahu na kupanga kuni juu yake. Kisha akamufunga Isaka mwana wake na kumulalisha juu ya kuni kwenye mazabahu.
Explorar Mwanzo 22:9
Início
Bíblia
Planos
Vídeos