1
Marko 5:34
Neno: Maandiko Matakatifu 2024
Isa akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako.”
Linganisha
Chunguza Marko 5:34
2
Marko 5:25-26
Hapo palikuwa na mwanamke aliyekuwa amesumbuliwa na tatizo la kutokwa damu kwa miaka kumi na mbili. Mwanamke huyu alikuwa ameteseka sana kwa mikono ya matabibu wengi, na kutumia kila kitu alichokuwa nacho. Lakini badala ya kupona, hali yake ilizidi kuwa mbaya.
Chunguza Marko 5:25-26
3
Marko 5:29
Mara kutoka damu kwake kukakoma, naye akajisikia mwilini mwake amepona kabisa.
Chunguza Marko 5:29
4
Marko 5:41
Akamshika mtoto mkono, akamwambia, “Talitha koum!” (maana yake, “Msichana, nakuambia: amka!”)
Chunguza Marko 5:41
5
Marko 5:35-36
Alipokuwa bado anaongea, watu wakafika kutoka nyumbani mwa Yairo. Wakamwambia, “Binti yako amekufa. Kwa nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?” Aliposikia hayo waliyosema, Isa akamwambia huyo kiongozi wa sinagogi, “Usiogope. Amini tu.”
Chunguza Marko 5:35-36
6
Marko 5:8-9
Kwa kuwa Isa alikuwa amemwambia, “Mtoke mtu huyu, wewe pepo mchafu!” Isa akamuuliza, “Jina lako ni nani?” Akamjibu, “Jina langu ni Legioni, kwa kuwa tuko wengi.”
Chunguza Marko 5:8-9
Nyumbani
Bibilia
Mipango
Video