Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

2 Wathesalonike 3:1-5

2 Wathesalonike 3:1-5 NENO

Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili Neno la Bwana Isa lipate kuenea kwa haraka na kuheshimiwa kila mahali, kama vile ilivyokuwa kwenu. Ombeni pia ili tupate kuokolewa kutokana na watu waovu na wabaya, kwa maana si wote wanaoamini. Lakini Bwana Isa ni mwaminifu, naye atawaimarisha ninyi na kuwalinda kutokana na yule mwovu. Nasi tuna tumaini katika Bwana Isa ya kuwa mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaagiza. Mwenyezi Mungu aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika saburi ya Al-Masihi.