Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Kumbukumbu 31:24-29

Kumbukumbu 31:24-29 NENO

Baada ya Musa kumaliza kuandika kwenye kitabu maneno ya sheria hii kutoka mwanzo hadi mwisho, akawapa Walawi wale waliolibeba Sanduku la Agano la Mwenyezi Mungu agizo hili, akawaambia: “Chukueni Kitabu hiki cha Torati mkakiweke kando ya Sanduku la Agano la Mwenyezi Mungu, Mungu wenu. Hapo ndipo kitakapokaa kama shahidi dhidi yenu. Kwa kuwa ninajua jinsi mlivyo waasi na mlivyo na shingo ngumu. Kama mmekuwa mkiasi dhidi ya Mwenyezi Mungu nikiwa bado niko hai na nikiwa pamoja nanyi, mtaasi mara ngapi baada ya kufa kwangu! Kusanyeni mbele yangu wazee wote wa makabila yenu na maafisa wenu wote, ili nipate kusema maneno haya masikioni mwao na kuziita mbingu na nchi ili kushuhudia dhidi yao. Kwa kuwa ninajua, baada ya kifo changu hakika mtakuwa waovu kabisa na kugeuka kutoka njia niliyowaamuru ninyi. Katika siku zijazo, maafa yatawapata, kwa sababu mtafanya maovu mbele za macho ya Mwenyezi Mungu, na kuchochea hasira yake kwa kazi za mikono yenu.”