Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Waefeso 6:10-13

Waefeso 6:10-13 NENO

Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana Isa na katika uweza wa nguvu zake. Vaeni silaha zote za Mungu ili mweze kuzipinga hila za ibilisi. Kwa maana kushindana kwetu si dhidi ya mwili na damu, bali dhidi ya falme na mamlaka, dhidi ya wakuu wa ulimwengu huu wa giza na majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. Kwa hiyo vaeni silaha zote za Mungu ili mweze kushindana siku ya uovu itakapokuja, nanyi mkiisha kufanya yote, simameni imara.