Waebrania 5:7-10
Waebrania 5:7-10 NEN
Katika siku za maisha ya Yesu hapa duniani, alimtolea maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, yeye awezaye kumwokoa na mauti, naye Mungu akamsikia kwa sababu ya kutii kwake kwa unyenyekevu. Ingawa alikuwa Mwana, alijifunza utiifu kutokana na mateso aliyoyapata, na akiisha kukamilishwa, akawa chanzo cha wokovu wa milele kwa wote wanaomtii. Naye amewekwa na Mungu kuwa Kuhani Mkuu kwa mfano wa Melkizedeki.