Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Hosea Utangulizi

Utangulizi
Hosea mwana wa Beeri alikuwa mzaliwa wa Ufalme wa Kaskazini, yaani, Israeli, ambao pia anauita Efraimu. Maana ya jina lake ni “Wokovu.” Inawezekana alianza huduma yake kabla ya kifo cha Mfalme Yeroboamu wa Pili mwaka wa 753 K.K. Huduma ya Hosea kwa Ufalme wa Kaskazini ilikaribiana sana na ile ya Amosi. Hawa wawili ndio manabii pekee wa Agano la Kale ambao vitabu vyao vilihusu Ufalme wa Kaskazini na maangamizi yake.
Hosea alipoanza huduma yake katika miaka ya baadaye ya utawala wa Yeroboamu wa Pili, Israeli ilikuwa inafurahia ustawi mkubwa wa kiuchumi na amani ya kisiasa iliyosababisha kuwepo kwa usalama pande zote. Mara baada ya kufa kwa Yeroboamu wa Pili mwaka 753 K.K., taifa lilianza kuharibika kwa haraka, na hatimaye likaangamia, nao Waisraeli wakapelekwa utumwani na Waashuru mwaka 722 K.K.
Mwandishi
Hosea mwana wa Beeri.
Kusudi
Kiini cha ujumbe wa Hosea ni kuonyesha upendo wa Mungu kwa watu wa Israeli waliogeuka na kumwacha Bwana.
Mahali
Ufalme wa Kaskazini (Israeli), ambao nabii anauita Efraimu.
Tarehe
715 K.K.
Wahusika Wakuu
Hosea, Gomeri, na watoto wao.
Wazo Kuu
Uhusiano wa Mungu na Israeli uliokuwa umefifia.
Mambo Muhimu
Hosea anaelezea hali ya taifa la Israeli akitumia hali iliyojitokeza katika maisha ya kila siku. Mungu anafananishwa na: mume, baba, simba, chui, dubu, umande, mvua, nondo, n.k. Israeli inafananishwa na: mke aliyekosa uaminifu kwa mumewe, mtu mgonjwa, mzabibu, mzeituni, mwanamke anayejifungua, jiko la kuokea, ukungu wa asubuhi, makapi, moshi, n.k.
Mgawanyo
Maisha ya Hosea katika familia (1:1–3:5)
Hali ya dhambi ya Israeli (4:1–6:3)
Adhabu kwa ajili ya Israeli (6:4–10:15)
Hukumu ya Mungu na rehema zake (11:1–14:9).

Iliyochaguliwa sasa

Hosea Utangulizi: NEN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia