Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Ayubu 35

35
Elihu alaumu mtu kujiona kuwa mwenye haki
1Ndipo Elihu akasema:
2“Je, unadhani hili ni haki?
Wewe unasema, ‘Nina haki mbele za Mungu.’
3Bado unamuuliza, ‘Ni faida gani nimepata,
na imenifaidi nini kwa kutokutenda dhambi?’
4“Ningependa nikujibu wewe
na rafiki zako walio nawe.
5Tazama juu mbinguni ukaone;
yaangalie mawingu yaliyo juu sana juu yako.
6Je, ukitenda dhambi, inamdhuruje Mungu?
Kama dhambi zako zikiwa nyingi,
hilo linamfanyia nini Mungu?
7Kama wewe ni mwadilifu, unampa nini,
au yeye anapokea nini mkononi kwako?
8Uovu wako unamdhuru tu mtu mwingine kama wewe,
nayo haki yako inawafaa wanadamu tu.
9“Wanadamu hulia kwa kulemewa na mateso;
huomba msaada kutoka mkono wenye nguvu.
10Lakini hakuna asemaye, ‘Yuko wapi Mungu Muumba wangu,
yeye anifanyaye niimbe usiku,
11yeye atufundishaye sisi zaidi ya wanyama wa nchi,
na kutufanya wenye hekima kuliko ndege wa angani?’
12Yeye hajibu wakati watu waliapo
kwa sababu ya kiburi cha watu waovu.
13Naam, Mungu hasikilizi maombi yao ya ubatili;
Mwenyezi hayazingatii.
14Si zaidi sana kwamba hatakusikiliza
wewe usemapo humwoni,
tena kwamba kesi yako iko mbele zake
na wewe lazima umngojee,
15pia zaidi, kwamba hasira yake kamwe haiadhibu
wala haangalii uovu hata kidogo?
16Hivyo Ayubu hufumbua kinywa chake kwa maneno yasiyo na maana;
anaongea maneno mengi bila maarifa.”

Iliyochaguliwa sasa

Ayubu 35: NENO

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia