Nehemia Utangulizi
Utangulizi
Vitabu vya Ezra na Nehemia vinakwenda sambamba na vitabu vya Mambo ya Nyakati, vikisimulia habari zinazofuata matukio ya Mambo ya Nyakati. Kitabu cha Nehemia kimepewa jina la mhusika wake mkuu ambaye ni Nehemia. Katika andiko la Kiebrania, kitabu hiki ni sehemu ya kitabu cha Ezra. Kuna uwezekano mkubwa sana kwamba katika kipindi hiki nabii Malaki alikuwa akihudumu.
Mwandishi
Kuna uwezekano mkubwa kwamba Nehemia au Ezra, au wote wawili ndio walioandika kitabu hiki, kwani mwanzoni Ezra na Nehemia vilikuwa kitabu kimoja.
Kusudi
Habari za kurudi kwa Wayahudi kutoka uhamishoni, na kujengwa kwa ukuta wa Yerusalemu.
Mahali
Yerusalemu.
Tarehe
Kuna uwezekano hiki kitabu kiliandikwa miaka ya 445–432 K.K.
Wahusika Wakuu
Nehemia, Ezra, Tobia na Sanbalati.
Wazo Kuu
Kitabu hiki kinaonyesha kutimizwa kwa unabii wa Zekaria na Danieli kuhusu kujengwa upya kuta za Yerusalemu.
Mambo Muhimu
Kujengwa kwa ukuta wa Yerusalemu, na kurejezwa kwa utaratibu wa ibada.
Mgawanyo
Nehemia anazijenga kuta (1:1–7:3)
Mabadiliko chini ya Ezra (7:4–10:39)
Mipango ya Nehemia (11:1–13:31).
Iliyochaguliwa sasa
Nehemia Utangulizi: NEN
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Biblia Takatifu™ Neno™
Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Version™
Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015 by Biblica, Inc.
Used with Permission. All Rights Reserved Worldwide.